Habari njema ya wokovu - Kuhesabiwa haki kutoka zambi
Michael Hardt


Maswali haya yanaambatana na Waroma 1 hadi 5,1. Na kipindi kitakachofwata kinazungumuza juu ya Waroma 5,12 hadi 8.
1.1 Maana ya neno «Injili» ama «Habari njema» ni gani ?
Tafsiri ya neno hili katika kiyunani ni «Habari Njema». Katika inchi ya Wayunani, wakati ushindi ulipatikana vitani, kulikuwa mjumbe aliyetumwa kupeleka habari mujini, na wakati alipokaribia muji alikuwa akisema kwa sauti kubwa eti «evangelion» : maana yake , habari njema- tumepata ushindi vitani ! Injili ni Habari njema ambayo Mungu alituma kutangaza tangu kufa na kufufuka kwake Kristo. Kuhusu yaliyomo, tazama swali linalofwata.
1.2 Injili inasema nini ?
Katika Biblia, Injili ao Habari Njema inatueleza namna gani Mungu alileta njia ya upatanishi katikati yake na mutu aliyekuwa amepotea. Njia hio ni katika Mwana wake Yesu, aliyekuwa Mungu tangu zamani hadi leo, aliyefanyika mutu na akafa msalabani kwa ajili ya wenye zambi : «Injili ya Mungu……iliyo katika Mwana wake» (Waroma 1,1,3). Yeye ndiye njia pekee ya kuongoza watu kwa Mungu (Matendo ya mitume 4,12). Mutu hakumtafuta Mungu, ila Habari Njema ni kwamba Mungu alimtafuta mutu mwenye zambi na anamupa wokovu kwa bure. (Angalia Luka 15)
1.3 Sababu gani Paulo hakuona haya kwa Habari Njema? (Waroma 1,16,17)
Ingewezekana Paulo aone haya kwa Habari Njema kwa sababu mutu, kwa kawaida, anapinga habari ya kumjulisha ya kwamba yeye ni mwenye zambi, na anazarau wenye kuleta habari kama hio, na anapendelea kuwapatisha haya.
Ila sasa Paulo yeye haoni haya yoyote kwa sababu zifatazo : ya kwanza, Habari Njema ni «uwezo wa Mungu» kwa yule anaeamini (16). Habari Njema ina nguvu ya kuwageuza watu na kuwapeleka kwa Mungu (kama wanakubali na kuamini). Tena, Habari Njema ni kwa watu wote (kwa Wayuda na kwa mataifa : Waroma 1,16). Na kwa mwisho, haki ya Mungu inaonekana(inafunuliwa) ndani ya hiyo Habari Njema.
1.4 Haki ya Mungu inafunuliwa namna gani katika Habari Njema ?
Habari Njema inaonyesha ya kwamba Mungu ni mwenye haki [1] : anapohukumu mwenye zambi katika hasira yake (Waroma 1,17,18), anapofufua Yesu (Waroma 4,25) na kumpatia nafasi ya heshima (Yoane 16,10), na wakati pia anaposamehe zambi za mwenye kutubu (1 Yoane1,9), anapohesbia haki wanaoamini Yesu (Waroma 3,25 ;4,5). Kwa hayo yote ni ya kushangaza kusikia ya kwamba wenye zambi waliokuwa chini ya hasira ya Mungu wanahesabiwa haki. Jibu kwa swali hilo linaonekana kwa Sw 1.11 na Sw 1.12.
1.5 Nani anaehitaji Habari Njema
Kila mtu. Paulo anagawa walimwengu kwa vikundi vitatu : watu waliopoteza kumjua Mungu wa kweli, na wakikataa nanmna yote ya kutembea kwa utaratibu (Waroma 1,18-32), wenye kujiwekea taratibu ya kuongoza njia zao (Waroma 2,1-16), na Wayuda (Waroma 2 ,17 hadi 3,9). Watu wote wanapatikana katika kimoja cha vikundi hivi vitatu. Na Paulo anaonyesha wazi ginsi gani watu wote hawa ni wenye hatia mbele ya Mungu.
1.6 Watu ni wenye zambi ? Hakuna hata mwenye haki mumoja?
Ni kweli kabisa, watu wote ni wenye zambi. Wale wa kikundi cha kwa kwanza, waliokataa namana yote ya utaratibu ni wenye zambi (hata kama hawakusikia Habari Njema) kwa sababu wangeweza kumjua Muumba wakitazama viumbe vya Mungu vinavyowazunguka, ila walikataa hayo. Wale wa pili nao walijifanyia sheria alakini hawakuziiheshimu na wakatenda kinyume ya zamiri zao (Waroma 2,15) . Waisraeli wao walikuwa na Sheria ya Mungu na waliikosea.
Na matokeo ni kwamba «hakuna mwenye haki, hata mumoja»(Waroma 3,10). « Kwa sababu wote wamefanya zambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu» (Waroma 3,23).
1.7 Basi hakuna suluhisho yoyote ?
Kuna suluhisho moja tu. Ili ufahamu waziwazi suluhisho hilo, ushike vema wakati wote ya kwamba Mungu anahukumu kwa haki, yeye ni mtakatifu na ni mwenye kuchukia zambi kabisa. Anajua kila moja wetu na kila zambi zetu. Halafu kuna njia mbili tu : Ao anapashwa kukuhukumu, ao unapashwa «kukuhesabia haki» mbele yake. Kwa kujua namana gani ile inaweza kufanyika, ninakusihi uone maswali yafuatayo.
1.8 « Kuhesabiwa haki» maana yake nini? (Waroma 3,20)
Kuhesabiwa haki maana yake ni «kuonekana bila kosa yoyote».Ni vema zaidi kuliko «pasipo kujua zambi. Ukihesabiwa haki unaweza kuonyesha Yesu Kristo anapokaa kwa kuume kwa Baba na kusema «mimi ni moja naye, alibeba zambi zangu na Mungu akakubali hivyo; ndiyo sababu mimi nimehesabiwa haki». Adamu mbele ya kutenda zambi kwake hangaliweza kusema hivyo.
Kama mutu fulani akitaka kukuhukumu kama mwenye zambi, anapshwa kumhukumu kwanza Kristo – na ile hayiwezekane.
Tukiwa tumehesabiwa haki, tangu wakati ule sisi ni wenye haki, ila haki hiyo haitoke kwetu sisi wala kwa mutu, ni haki ya Mungu tuliopewa (tuliotolewa) – angalia Waroma 4,3,5,11 na Wafilipi 3,9
1.9 «Matendo ya sheria» ni nini (Waroma 3, 20)?
Matendo ya sheria siyo tu yale yanayohusu kushika sheria ya Musa , lakini ni matendo yanayohusu kushika sheria yoyote. Ile ambayo Waisraeli walionyesha mbele ya sheria ya Musa inaonyesha kwamba hakuna mutu anayeweza kuheshimu sheria yoyote. Ile ni kwa watu wote. Hakuna tendo lolote mutu anaweza akatenda ili ahesabiwe haki mbele ya Mungu.
1.10 Ni namna gani mutu anaweza kuhesabiwa haki mbele ya Mungu (Waroma 3,22-23)?
Kwa ngambo yetu sisi ni kwa njia ya imani tu. Na kwa ngambo ya Mungu ni kwa neema tu. « Kwa njia ya imani» inamaanisha kwamba tunamutegemea Yesu aliyelipa bei ya zambi zetu na malipo haya yanatosha. «Kwa neema» inamaanisha tunaweza kupokea tu ao kusadiki ile ambayo Mungu alitenda,lakini hatuwezi kuongeza kitu ao kujifanyia jambo lolote.
Kwa njia ya damu ya Yesu, Mungu alituhesabia haki, ndiyo maana ya neno hili «imani kwa njia ya damu yake» : Bwana Yesu alikufa pahali petu.
1.11 Neno hili «ambaye Mungu amekwisha kumuweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake» (Waroma 3,25) tunalisikia namana gani ?
Katika Kiebrania neno linalosema «upatanisho » lina maana ya «kitu kinachofunika»(ona Sw 2.7). Katika Agano la Kale, ilikuwa ni mufuniko wa sanduku la agano; uliotengenezwa katika zahabu, inayomaanisha haki ya Mungu. Mawe ya amri za Mungu,(ambayo yanaonyesha kila mara ya kwamba mutu ni muovu) yalikuwa katika sanduku la agano. Makerubi (walinzi wa utakatifu wa Mungu, wenye kutimiza hukumu ya Mungu; Mwanzo 3,24) walikuwa wakiinama juu ya ilie sanduku ya agano(Kutoka 25,20 na 37,9) , kwa namna hiyo walionyesha ya kwamba wanaitika kama Mungu alihukumu mwanadamu. Ila mufuniko huo ulikuwa na damu iliomwangwa juu yake (Walawi 16,14,15), damu ya nyama asiyekuwa na kasoro yoyote, iliyomwangwa kwa ajili ya watu waovu. Kwa hivyo Mungu aliokoa watu wake. Ni mfano wa ile Yesu Kristo alitenda: alitoa uzima wake mwenyewe, damu yake ikamwangwa, kwa hayo Mungu hatuhukumu tena.
Tafsiri fulani zinatumia neno «utakaso» pahali pa «upatanisho»katika Waroma 3,25 lakini tunapashwa kujua kabisa ya kwamba kazi ya utakaso ilifanyika pale msalabani katika tendo la utakaso na kufa kwa Bwana Yesu. Mufuniko wa hiyo sanduku ya agano ni ni njia ya utakaso, yaani Yesu mwenyewe. Kuketi kwake kwa kuume kwa Baba milele na milele, inahakikisha uwezo wa kazi yake. Neno “utakaso” linatumiwa sana katika luga ya kifaransa kuliko neno “upatanisho, lakini neno upatanisho linaonyesha vizuri zaidi ya kwamba zambi yetu zilifunikwa na mutu mwengine aliyepata gazabu yetu yote. Zambi zetu hazikufunikwa na sisi wenyewe. Kristo ndiye aliazibiwa :na yeye ndiye aliyetakasa zambi zetu zote (2 Yoane2:2)
1.12 Namna gani Mungu anaweza kuhesabu haki mwenye zambi na yeye anabaki mwenye haki ?
Kwa sababu Kristo alikamata nafasi yetu yaani alipokea hukumu ya zambi tuliyostahili. Kama unalipa deni yangu, muhukumu atafanya tena nini juu yangu? Hakuna ! Kuna mwenye alinilipia. Hakuna mutu yeyote ambaye angeliweza kupata ginsi ya kulipa kama hii ili nihesabiwe haki na kusamehewa. Hiyo ndiyo habari ya ajabu. Mungu anasamehe (ni jambo la ajabu), Lakini Mungu «haachilie» zambi kupita bure. Anatoa masamaha nyuma ya kuhukumu makosa na kuazibu zambi. Tatizo lilipata suluhisho, lakini kwa namna ya haki.
1.13 Ilikuwa namna gani kwa watakatifu wa Agano la Kale ? Walihesabiwa haki namna gani (Waroma 4) ?
Sawasawa na waamini wa Agano Jipya : ni kwa njia ya imani. Abrahamu aliamini Mungu, na kuwa alikubali neno lake Mungu akahesabiwa haki (Waroma 4,3).Mungu alimuhesabia haki kwa njia ile kwa sababu alitazamia toleo (lililokuja nyuma) la Yesu : Waroma 3,25,26.
1.14. Mbona Yakobo anasema ya kwamba Abrahamu alihesabiwa haki kutokana na matendo ?
Ndiyo kweli. Alakini Yakobo anafasiria namna kuhesabiwa haki kwetu kunatokana na imani pia na wema : kuhesabiwa haki hiyo inapashwa kuonekana wazi kwa matendo yanaotambulikana na wote (Yakobo 2,21). Abrahamu aliweza kuonekana kuwa mwenye haki namna gani ? ni kwa matendo yake. Wakati alikwenda kumtoa mwana wake Isaka ndipo alionyesha wazi wazi yakuwa ni mwenye imani. Ila Mungu yeye alikuwa anajua, mbele ya hapoi, ya kuwa Abrahamau ana imani. Na basi Mungu akahesabia haki kwa Abrahamu (Mwanzo 15,6,7).
1.15 Sababu gani Kristo alipashwa kufufuka ili tuhesabiwe haki (Waroma 4,25) ?
Kazi Kristo aliyoifanya ilitimia wakati alisema kwa sauti kubwa «imekwisha », akatoa roho na akafa (Yoane 19,30) lakini kwa ufufuko wake , Mungu alipendelea kuonyesha kwa macho ya wote (watu na malaika) yakwamba kifo cha Kristo kimekubaliwa kwake na kimetosha kabisa.
Mungu alitosheka kikamilifu na kazi yake (Waroma 4,25). Tokea hapo Mungu alibaki mwenyi haki na akahesabia haki wale wanaoamini Yesu (Waroma 3,26), ndiyo wale wanaoweka tumaini lao katika kazi ya Yesu msalabani. Na Kwa sababu Kristo alifufuka, tunajuwa kweli ya kwamba kazi ya Yesu msalabani ilikubaliwa na Mungu, na imani yetu inahakikishwa.
1.16 Kuhesabiwa haki kuna matokeo gani (Waroma 5,1,2) ?
Tuna amani pamoja na Mungu (Waroma 5,1), sasa hakuna tatizo katikati yetu na Mungu !Hiyo si ahadi ya siku za usoni – mwamini anakuwa na amani hiyo tangu sasa ! Hakuna tena kitu chakuzuiya uhusiano wetu na Mungu. Si kwa sababu hakuna tena mabaya ndani yetu, ni kwa sababu tupo ndani ya neema yake tu (mustari wa 2) : Mungu ni kwa upande wetu (Waroma 8,31) ; ana mawazo mazuri juu yetu.
1.17 Ile yote inaonekana namna gani katika maisha yetu ya kila siku ?
Mistari ifuatyo (Waroma 5,3 – 11) inatuonyesha ya kwamba hata katika ziki (matatizo, magumu makubwa) yale tunayopitia kila siku maishani mwetu tunapashwa kuyafurahia, na yanatuletea uvumilivu, kuelewa mambo ya maisha hata tumaini. Roho Mtakatifu amemimina upendo wa Mungu ndani ya roho zetu. Upendo huo, Mungu ameuonyesha wakati Kristo alikufa kwa ajili yetu – wakati tulikuwa bado wenye zambi. Kwa mwisho : kama Mungu alitutendea yote tuliyohitaji wakati tulikuwa tungali adui zake, na sasa hivi tuko katika upatanisho na kupendwa naye hatazidi kutuokoa katika magumu ya kila siku na kutuepusha na hasira itakayokuja ? Huo ni uhakika mkubwa !
[1] Mungu ni mapendo (1 Yoane 4,16) lakini yeye vile ni nuru (1 Yoane 1,5)